TAMKO LA RSA KUHUSU AJALI NA HALI YA USALAMA BARABARANI
Mwenyekiti Baraza la Taifa la Usalama Barabarani; Watanzania wote kwa ujumla; Napenda kuchukua nafasi hii, kwa niaba ya mabalozi wa usalama barabarani, kuungana nawe na watanzania wote kutoa pole kwa wafiwa na majeruhi wa ajali ya basi la Majinja Express iliyotokea huko Mafinga mkoani Iringa tarehe 11.03.2014 na kuwapoteza watu 50 na kuacha wengine wengi majeruhi. Ajali hii ni ya kustua na kusikitisha sana. Poleni majeruhi na Mwenyezi Mungu awajalie majeruhi uponyaji wa haraka na marehemu awapokee kwenye nuru ya uso wake. Road Safety Ambasadors(RSA) ni mtandao wa wananchi waliohamasika katika kusaidiana na kikosi cha usalama barabarani kutii sheria bila shuruti, kuelimisha umma kuhusu usalama barabarani, na kuripoti matukio mbalimbali barabarani ikiwa ni pamoja na kufichua mwenendo mbaya wa madereva na askari barabarani. Tufanya kazi zetu kupitia mtandao wa kijamii wa whatsapp,telegram (RSA-Kulikoni Barabarani)and facebook-Nenda kwa Usalama Barabarani. Pia tunatoa elimu kwa umma kupitia redio na televisheni. Ni mtandao wa hiyari wenye lengo la kupunguza ajali za barabarani na madhara yake kwa jamii. Kwa miaka mingi sasa ajali za barabarani zimeendelea kukatisha maisha ya watanzania walio wengi na kuwaachia wengi uyatima na ulemavu. Takwimu zinaonesha kuongezeka kwa ajali tangu ajali 6410 (1977) hadi kufikia 20618(2008; 23842(2013). Ni mwaka 2014 tu ndipo ajali zilipungua kufikia 14360 zilizosababisha vifo 3750 ukilinganisha na vifo 2905(2008) na vifo 878(2007). Tunapongeza hatua zilizofanyika kupunguza ajali mwaka 2014 japokuwa idai ya vifo ilikuwa bado iko juu ukilinganisha na 2008. Hatua mbalimbali zimetangazwa kuchukuliwa na serikali, lakini ufanisi wa hatua hizo bado umekuwa wenye mashaka. Mara nyingi kila ajali inapotokea jibu la haraka limekuwa mwendo kasi wa dereva na tukishatoa salamu za rambi rambi tu tunasahau kabisa bila hata kujua hatima ya waathirika wa ajali hizo. Hatukatai, ni kweli makosa ya kibinadamu inasemekana yanachangia sana hizi ajali. Hata hivyo ipo haja ya kwenda mbali zaidi ya majibu mepesi kuwa ni mwendo kasi tu. Twende mbele zaidi tufuatilie na kuweka utaratibu mzuri kuhusu haki za waathirika baada ya ajali. Wengi wamekuwa hawapati haki zao kabisa au hupata kwa kuchelewa jambo linalopelekea kuwapa machungu zaidi majeruhi na hata yatima na wajane wanaobaki baada ya ndugu zao kufariki. Ifike hatua tuache kutoa majibu mepesi kwa maswali magumu na kuchukua hatuia stahiki ili kukabiliana na hali hii.
Sisi kama mtandao wa mabalozi wa usalama barabarani(RSA) tunaitaka serikali
na wadau wanaohusika kuchukua hatua za makusudi kukabiliana na hali hii hasa zinapotokea ajali kubwa. (Major accidents) 1.
2.
3.
4.
5.
6.
7.
Kuundwa kwa taasisi huru na ya kitaalamu (National Road Accidents
Investigation Board)kuchunguza kwa kina ajali husika ili kubaini chanzo halisi cha ajali hiyo na vitu vilivyochangia. Katika kuangalia Nini kilitokea; Namna gani kilitokea; Kwa nini kilitokea; Nini kifanyike kuzuia kujirudia; na Kipi kifanyike kupunguza athari ya ajali, bodi iangalie yafuatayo: (a) Iwapo TANROADS wana program ya ukaguzi wa mara kwa mara wa barabara na kuzifanyia marekebisho (b) Iwapo mabasi yanayohusika kwenye ajali yanakuwa na bima sahihi na inayotosha kufidia wahanga wa ajali hizo (c) Iwapo kila mamlka ilitekeleza wajibu wake kabla na baada ya kutokea kwa ajali (d) Uwepo wa bajeti ya kutosha kufanya matengenezo ya barabara na kama ipo kwa nini ukarabati haukufanyika kwa wakati (e) Iwapo wamiliki wa mabasi wana sera na taratibu zozote za kukabiliana na ajali na nidhamu za watumishi wao (f) Mafunzo ya dereva husika aliyepata ajali, historia ya maisha yake, na siku kabla ya ajali au wakati wa ajali hali ya akili yake ilikuwaje. (g) Nafasi ya hali ya kijiografia katika ajali husika mathalani, uoni, muundo wa kijiografia wa eneo hilo, hali ya hewa nk (h) Mwendo wa gari husika na hali ya gari hadi wakati wa ajali (roadowrthiness) (i) Abiria kwa kiasi gani walichangia mwendo mbaya kwa kutoripoti na je iwapo waliripoti ni hatua gani zilichukuliwa dhidi ya dereva au abiria husika. Kuwawajibisha wote watakaobainika kwa namna moja ama nyingine kuchangia kusababisha ajali. Hii ihusishe uwajibikaji wa mamlaka mbalimbali kama vile Polisi Usalama Barabarani, SUMATRA, TANROADS, na Wamiliki wa Magari husika. Bima za magari ya abiria na ya mizigo zichunguzwe ili kuona kama zinakidhi vihatarishi(risks) vinavyoweza kusababishwa na magari hayo, uhai na uhalali wa bima hizo na ukubwa fidia zinazotolewa na bima hizo (coverage) Shule za udereva na sheria zake ziangaliwe upya ili kuona kama shule hizo zinakidhi mafunzo ya udereva kulingana na teknolojia ya sasa ya maendeleo ya magari na hasa mitaala inayotumika. Mfumo wa upatikanaji leseni uangaliwe kwa kina kuona kama hauna mianya ya kuwafanya watu wapate leseni bila kupitia mafunzo au kufuzu vizuri na ikiwezekana mamlaka inayojitegemea ya utoaji leseni na ukaguzi wa magari ianzishwe kama ilivyoanishwa kwenye sera ya usalama barabarani, 2009. Kutungwa kwa sheria ya Mauaji ya bila kukusudia yanayosababishwa na taasisi (Corporate manslaughter Act) kama ilivyo kule UK ili kuziwajibisha taasisi zisizojali usalama wa watu. Kutekeleza kwa vitendo malengo ya sera ya usalama barabarani, 2009, na kuweka adhabu kali kwa wanaokiuka sheria za usalama barabarani
8. 9.
Kuweka utaratibu mzuri wa kushughulikia malipo ya fidia ya bima kwa
waathirika wa ajali Kutumia teknolojia ya kisasa ya ufuatiliaji magari ya abiria barabarani(Real Time Traffic Monitoring System).
Tunaamini kuwa haya yakitekelezwa vyema, tunaweza kupunguza ajali kwa
kiwango kikubwa sana. Sisi kama mabalozi wa usalama barabarani tutaendelea kutii sheria bila shuruti na kuendelea kwa nguvu zetu zote kutoa elimu ya usalama barabarani kila siku kupitia mbinu mbalimbali. RSA tunalaani mtu au taasisi yoyote iliyoshindwa kutekeleza wajibu wake na kupelekea au kuchangia kwa namna moja au nyingine kutokea kwa ajali hii. JOHN SEKA Mwenyekiti-RSA rsatza@gmail.com PAMOJA TUNAIMARISHA USALAMA BARABARANI
Madhara Yatokanayo Na Ajali Za Barabarani Yamemeendelea Kuwa Sababu Namba Tisa Katika Kusababisha Vifo Vya Watu Wengi Zaidi Duniani Ambapo Inakadiriwa Zaidi Ya Watu Milioni 1
Hotuba Ya Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi Na Mawasiliano Mheshimiwa Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe (Mb), Akiwasilisha Bungeni Mpango Na Makadirio Ya Mapato Na Matumizi Ya Fedha Kwa Mwaka Wa Fedha 2019_2020
HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA
MIZENGO PETER PINDA (MB), KUHUSU MAPITIO NA MWELEKEO WA KAZI ZA SERIKALI NA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA OFISI YA WAZIRI MKUU NA OFISI YA BUNGE KWA MWAKA 2014/2015