You are on page 1of 5

HOTUBA YA MHE. DKT.

MOHAMMED GHARIB BILAL, MAKAMU WA


RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KILELE
CHA MAADHIMISHO YA 27 YA WIKI YA MAJI MKOANI MARA
TAREHE 22.03.2015
Mheshimiwa Prof. Jumanne A. Maghembe (Mb)
Waziri wa Maji;
Mheshimiwa Prof. Peter Msolla
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji;
Mheshimiwa Kapteni Mstaafu Aseri Msangi
Mkuu wa Mkoa wa Mara;
Mheshimiwa Malika Berak,
Balozi wa Ufaransa Nchini Tanzania;
Waheshimiwa Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa;
Inj. Mbogo Futakamba
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji;
Waheshimiwa Wabunge na Madiwani wa Mkoa wa Mara na Mikoa Jirani;
Viongozi wa Vyama vya Siasa na Serikali;
Washirika wetu wa Maendeleo katika Sekta ya Maji;
Ndugu Wananchi;
Mabibi na Mabwana

Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, kwa kutuwezesha


kukutana hapa siku ya leo katika Kilele cha Maadhimisho ya 27 ya Wiki ya
Maji Kitaifa kwa mwaka 2015 yanayofanyika Mkoani Mara. Namshukuru sana
Waziri wa Maji, na Mkuu wa Mkoa na Wananchi kwa kunipa heshima kubwa
ya kunialika nije kuungana na wananchi wa Manispaa ya Musoma na
Watanzania kwa ujumla kushiriki katika Kilele cha Maadhimisho haya
yanayofanyika hapa katika Viwanja vya Mkendo mjini Musoma. Vilevile,
niwashukuru wananchi wote wa Mkoa wa Mara kwa mapokezi mazuri
waliyonipatia Nasema Asanteni Sana.
Ndugu Wananchi;

Leo hii nchi yetu inaungana na nchi nyingine kote duniani kuadhimisha Siku
ya Maji Duniani, ambayo ndiyo kilele cha Wiki ya Maji kwa hapa nchini.
Kaulimbiu ya Maadhimisho ya Wiki ya Maji kwa mwaka huu wa 2015 ni Maji
Kwa Maendeleo Endelevu, ambayo inakwenda sambamba na umuhimu na
mchango wa Sekta ya Maji kwa Maendeleo ya Sekta nyingine za Kiuchumi na
Kijamii.
Tumeanza leo kwa kuweka Jiwe la Msingi katika Mradi mkubwa wa Maji hapa
Mjini Musoma, na mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Aprili, 2015 na
utagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 41. Ni mategemeo yetu kuwa Manispaa

ya Musoma itakuwa na maji ya uhakika kwa asilimia 100 baada ya mradi huu
kukamilika. Tena, mafanikio yatakayopatikana kutokana na kukamilika kwa
mradi huu ni pamoja na:
(i)
Kuongezeka kwa uzalishaji wa maji kutoka mita
za ujazo 10,000 za
sasa kwa siku, hadi mita za ujazo 36,000 kwa siku.
(ii)
Kupanua huduma ya maji katika baadhi ya
maeneo ambayo hayana huduma, na maeneo ya mpakani mwa
Manispaa ya Musoma kama vile Bisumwa, Etaro na Nyabange.
(iii)
Ubora
wananchi utaongezeka
magonjwa.

wa
maji yanayosambazwa kwa
na hivyo kupunguza milipuko ya

(iv)
Kuongezeka kwa mapato ya Mamlaka mara
mbili yatakayosaidia kuimarisha na kustawisha huduma endelevu
ya maji kwa wakazi wa Manispaa ya Musoma.
(v)
Kuimarika kwa huduma ya maji kwenye
maeneo yote ya Manispaa ya Musoma na maeneo yaliyokuwa
yanapata maji kwa mgao kama vile Buhare, Kigera Rwamlimi, na
Bweri.
(vi)
Muda wa utoaji wa huduma ya majisaf
utaongezeka kutoka wastani wa saa 22 kwa siku za sasa
hadisaa 24 kwa siku.
Naomba nitoe rai kwa Wananchi wa Manispaa ya Musoma na Mkoa wa Mara
kwa ujumla, tuutunze mradi huu na miradi yote inayoendelea kutekelezwa
ili iendelee kuwasaidia ninyi na vizazi vijavyo.
Ndugu Wananchi;

Sekta ya Maji kama Sekta nyingine imeendelea kukua kwa kadri ya


maendeleo ya nchi yetu kijamii na kiuchumi. Imetoa mchango mkubwa
katika ustawi wa jamii zetu mijini na vijijini kwa afya za wananchi na
matumizi ya majumbani; maendeleo ya kiuchumi katika kilimo, viwanda,
utalii, usafri na usafrishaji; na kubwa zaidi ni umuhimu wa maji katika
utunzaji wa mazingira na hali ya hewa. Maji yana umuhimu mkubwa katika
ustawi na maendeleo ya Taifa lolote lile hapa duniani.
Hivi karibuni tumeshuhudia ongezeko kubwa la mahitaji ya maji kwa
matumizi ya nyumbani katika miji yetu. Vilevile, sote tunaona mahitaji
makubwa ya maji katika uzalishaji wa chakula; uzalishaji wa bidhaa za
viwandani; uzalishaji wa nguvu za umeme kwa kutumia nguvu za maji, na
kuongezeka kwa uzalishaji katika nyanja za gesi na mafuta; na matumizi ya

rasilimali ya maji katika mazingira. Hii ina maana kwamba matumizi ya


rasilimali maji yasiyo endelevu yana athari kubwa kwa mazingira. Hivyo,
kuna umuhimu mkubwa wa kutunza mazingira yetu, ili tuendelee kupata
huduma endelevu ya maji.

Ndugu Wananchi;

Takwimu zilizopo zinatia hofu; kati ya mwaka 2000 hadi mwaka 2050,
mahitaji ya maji kidunia yataongezeka kwaasilimia 55. Hali hii itasababisha
kuongezeka kwa migogoro ya matumizi ya maji baina ya watumiaji wa
rasilimali za maji. Nitoe rai kwa Wataalam wa Sekta ya Maji pamoja na Sekta
nyingine zinazohusiana, kuhakikisha kuwa wanatafuta suluhisho la
upatikanaji wa maji, nishati, na uhakika wa chakula na kuwa na mipango
makini, matumizi ya teknolojia sahihi na kubwa zaidi ni ushirikiano wa karibu
baina ya wadau mbalimbali wa maji. Na juu ya haya yote, ni msisitizo katika
utunzaji endelevu wa mazingira yetu ili yaendelee kutuhifadhi. Aidha,
teknolojia za uvunaji wa maji ya mvua na ujenzi wa mabwawa ni maeneo
ambayo yatatuhakikishia kwamba tunakuwa na huduma endelevu ya
rasilimali ya maji.
Ndugu Wananchi;

Maji ni rasilimali inayotumika sana, na ni msingi wa upatikanaji wa karibu wa


kila huduma inayotolewa humu duniani. Katika karne ya 20, idadi ya watu
duniani
imeongezeka mara
nne zaidi wakati
mahitaji
ya
maji
yameongezeka mara tisa zaidi. Kasi hii ya ongezeko la matumizi ya maji,
pamoja na sababu nyingine imeathiri hali ya upatikanaji wa maji. Mwaka
2014, Jukwaa la Uchumi Duniani liliazimia kuwa uhakika wa upatikanaji wa
maji ni moja ya changamoto zinazokuwa kwa kasi duniani. Sisi kama nchi
hatuna budi kuwa na mikakati ya makusudi kukabiliana na changamoto hizo,
jambo ambalo Serikali imeanza kulifanyia kazi.
Uhaba wa maji na kutopatikana kwake kwa uhakika kunaleta athari mbaya
katika shughuli zote za kiuchumi. Utoaji wa huduma ya maji usiosimamiwa
ipasavyo na kwa umakini unaleta changamoto kubwa za kiuchumi na kijamii.
Hivyo basi, usimamizi mzuri wa rasilimali za maji utakuwa chachu na chanzo
cha maendeleo ya haraka ya jamii na Taifa letu. Kwa sababu ya umuhimu wa
maji kwa shughuli za kiuchumi za nchi yetu; upungufu au makosa yoyote
yatakayofanyika katika mipango, usimamizi na matumizi yanaweza kuwa na
athari za muda mrefu kwa jamii na nchi. Hali hii inaweza kwenda mbali zaidi,
hata kuziathiri nchi za jirani tunazochangia nazo rasilimali za maji.
Mfano wa karibu ni hapa kwetu Mkoa wa Mara, Mto Mara unaanzia safari
yake ya kuingia Ziwa Victoria kutokea nchi jirani ya Kenya; hivyo kama kuna
mipango duni, basi athari zake zitaonekana kwenye nchi zote mbili.

Ndugu Wananchi;

Sekta ya Maji inayoratibiwa na Wizara ya Maji bado ina jukumu kubwa la


kuhakikisha miji na hasa vijiji vyetu, vinapatiwa huduma ya maji saf na
salama na huduma ya usaf wa mazingira katika umbali usiozidi mita 400, ili
akinamama na dada zetu waondokane na maisha yenye kuonekana yana
suluba. Tusisahau ule msemo wetu, Maji ni Uhai, Usafi wa Mazingira ni
Utu na Utunzaji wa Vyanzo vya Maji ni Ustaarabu.
Mabadiliko ya tabianchi kupitia uwepo au uhaba wa maji yanaathiri
binadamu, jamii na mazingira. Usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji
ulio makini na endelevu ni muhimu katika kukabili athari mbaya za
mabadiliko ya hali ya hewa. Isitoshe, maji yana mchango mkubwa katika
kukabili mabadiliko ya hali ya hewa, kwani upatikanaji wa uhakika wa
rasilimali za maji unapunguza kwa kiasi kikubwa uchafuzi wa hali ya hewa.
Majanga yanayohusiana na maji kama vile, mafuriko na ukame kwa kiwango
kikubwa ni maafa yanayojitokeza mara nyingi katika sehemu mbalimbali
duniani hivi sasa. Vifo, uharibifu wa mali, makazi na miundombinu vina athari
kubwa kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja, kikundi, jamii na hata Taifa.
Katika miaka ya hivi karibuni, tumeshuhudia ongezeko la wingi na athari
mbaya za majanga haya. Hivyo, kusababisha kuwepo kwa uhaba mkubwa wa
rasilimali za maji kwenye baadhi ya maeneo. Kwa mfano, athari zimeshaanza
kuonekana katika uzalishaji wa nishati ya umeme katika vinu vya kufua
umeme vya Kidatu, Mtera, Hale na Nyumba ya Mungu. Vilevile, kasi ya
kupungua kwa maeneo ya misitu yetu kwa hivi sasa ni kubwa.
Ndugu Wananchi;
Hivyo, bila ya kuwa na mipango mikubwa ya pamoja kwa sekta zote ili
kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa, majanga haya yatazidi
kuongezeka. Natoa wito kwa wadau wote kujiunga pamoja katika kukabiliana
na athari mbaya za mabadiliko ya hali ya hewa. Kwani, mabadiliko haya yana
athari kuanzia kwenye kupungua kwa misitu na vyanzo vya maji; kupungua
kwa rasilimali za maji juu na chini ya ardhi; kuathirika kwa ubora wa maji ya
kunywa; hadi kukua kwa utoaji wa gesi ya ukaa. Athari hizi zinakwenda mbali
kwenye maendeleo ya jamii zetu na Taifa kwa ujumla.
Ndugu Wananchi;

Mwenendo wa mvua kwa kiasi kikubwa unaathiriwa na mabadiliko haya ya


hali ya hewa, na wakati huohuo mahitaji ya rasilimali maji yanaongezeka.
Kulingana na takwimu za Shirika la Chakula Duniani (FAO) inatarajiwa
kwamba ifkapo mwaka 2050, asilimia 60 zaidi ya chakula kitahitajika ili
kulisha idadi ya watu watakaoongezeka duniani. Hivi sasa, watu milioni
800 wana lishe duni na wengi wao wanatoka kwenye jamii zenye vipato
duni.
Hivyo, wataalam wa sekta zote wana jukumu kubwa la kutumia taaluma zao
ili kuwa na matumizi bora ya maji kwa upatikanaji wa mavuno makubwa ya

chakula. Hapa nisisitize kwamba matumizi ya njia za kilimo zisizo na tija na


ufanisi, zitasababisha matumizi makubwa ya maji. Kwa hiyo basi, kuna
umuhimu wa kuandaa sera thabiti na makini katika kushughulikia masuala
haya ili matumizi ya maji yafanywe kwa ufanisi.
Ndugu Wananchi;

Serikali yetu itaendeleza juhudi za kuhakikisha tunawafkishia wananchin


wetu maji saf na salama katika maeneo ya nchi yetu. Naamini inawezekana
kabisa kuongeza huduma ya maji kwenye maeneo ambayo hivi sasa haipo
au haitoshelezi mahitaji. Tunajua kuwa ipo changamoto kubwa hasa vijijini
lakini kinachohitajika zaidi ni ushirikiano kutoka kwa wadau wetu wote
wakiwemo wananchi, Washirika wa Maendeleo, Vyama Visivyo vya Kiserikali
na vya Kijamii, na Uongozi wa Serikali katika ngazi zote.
Napenda kusisitiza kuwa dhamana kubwa kwenu wananchi ni kutoa mchango
unaostahili katika usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji. Pia, tunalo
jukumu kubwa la kutunza vyanzo vya maji popote pale vinapopatikana. Ili
kuongeza ufanisi wa kutekeleza mipango yenu, nawashauri mshirikiane kwa
karibu zaidi na sekta zote zinazohusiana na Sekta ya Maji; na vilevile,
watumiaji wa maji wakubwa na wadogo nchini ili kuepusha migogoro ya
kugombea maji.
Ndugu Wananchi;

Mwisho kabisa napenda tena kutoa shukrani kwa Uongozi wa Wizara ya Maji
na Mkoa wa Mara kwa kunialika kushiriki nanyi kwenye Kilele cha
Maadhimisho ya 27 ya Wiki ya Maji Kitaifa. Napenda pia, kuwashukuru wote
walioshiriki kwenye Maonesho ya Wiki ya Maji na kuwapongeza Washindi wa
Maonesho hayo. Niwashukuru pia wale wote waliochangia katika kuandaa
Maadhimisho ya mwaka huu, ikiwa ni pamoja na Wadau wetu wa
Maendeleo. Naipongeza pia Kamati ya Maandalizi kwa kazi yao nzuri
iliyohakikisha maadhimisho yanafanyika katika hali ya usalama na amani.
Baada ya kusema hayo, ninayo furaha sasa kutamka kuwa
Maadhimisho na Maonesho ya 27 ya Wiki ya Maji Kitaifa
yamefungwa rasmi.
ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA

You might also like