Professional Documents
Culture Documents
ugawaji wa dawa hizi. Kabla ya unywaji wa Dawa hizi Mtoto anatakiwa ale
chakula na katika muda usiozidi masaa 2 baada ya kula awe amepatiwa
dawa hizi; chakula hicho kitaandaliwa shuleni.
Hivyo kila Mzazi katika mkoa wa Mwanza anaombwa amruhusu mtoto
wake aende kumeza dawa hizi muhimu ili ajikinge na kupata tiba ya
magonjwa haya hatari kwani huduma hii ya dawa za kinga tiba inatolewa
bila malipo kwa kila mtoto.
Dawa hizi zimethibitishwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuwa ni
salama, na hazina madhara yoyote kwa afya ya binadamu zinapomezwa
kwa kufuata maelekezo yanayotolewa na wahudumu wa afya na Walimu
waliopatiwa mafunzo.
Dawa zitakazohusika ni za Praziquantel za kudhibiti Kichocho na
Albendazole za kudhibiti Minyoo ya tumbo ambazo zitatolewa kwa watoto
wote wenye umri wa kwenda shule, walioandikishwa na ambao
hawakuandikishwa.
Ndugu Wananchi,
Ni matumaini yetu
wingi ili kumeza dawa hizi kwa maendeleo ya afya za watoto wetu na Jamii
kwa ujumla. Nawaombeni sana, muendeleze sifa nzuri ya Mkoa wetu kwani
umekuwa ukifanya vizuri miaka yote katika suala zima la chanjo.
Asanteni sana kwa kunisikiliza.
IMETOLEWA NA OFISI YA MKUU WA MKOA MWANZA