You are on page 1of 3

MKATABA WA KUTUNZA SHAMBA

Mkataba huu unafanyika leo tarehe ______ Mwezi . 2013


KATI YA
Winners Group wa S.L.P.., Dar es Salaam (ambaye hapa ataitwa
Mmiliki neno ambalo litamhusu yeye, ndugu, mawakala au warithi wake)
kwa upande wa mmoja;
NA
.., wa S.L.P. .., Dar es Salaam (ambaye
hapa ataitwa Mtunzaji neno ambalo litamhusu yeye, ndugu, mawakala au
warithi wake) kwa upande wa pili.
KWA KUWA Mmiliki wana uhalali wa kumiliki shamba heka 10 lililoko kijiji
cha Fukayosi wilaya Bagamoyo mkoa wa Pwani;
KWA KUWA Mmiliki wanayo nia ya kumpa mtunzaji mamlaka ya utunzaji wa
shamba kwa maelewano na masharti yaliyopo hapa chini;
KWAHIYO wote Mmiliki na Mtunzaji wanataka kuweka makubaliano na
masharti yao katika mkataba rasmi;.
BASI MAKUBALIANO HAYA YANASHUHUDIA KAMA IFUATAVYO: 1. Kwamba Mmiliki atamlipa Mtunzaji kiasi cha Shilingi za Kitanzania
. kwa mwezi kwa kutunza shamba tajwa hapo juu.
2. Kwamba mkataba huu utadumu kwa muda wa ambao
utaanza tarehe .. na kuishia tarehe ..
3. Kwamba Mtunzaji hatapangisha shamba hilo au sehemu yoyote ya
shamba kwa mtu mwingine yeyote yule na endapo kutakuwa na haja
ya kufanya hivyo basi Mtunzaji atawajibika kuomba kibali cha
maandishi kutoka kwa Mmliki.
4.

Kwamba Mtunzaji atatumia shamba hilo kwa shughuli za Mmiliki tu na


kamwe haitatumika kufanya shughuli za Mtunzaji za binafsi, pamoja
na kuangalia mazao yote yaliyopandwa ndani ya shamba hilo, kama
ufuta, mananasi, maembe , miti ya mipira nk

5.

Kwamba Mtunzaji atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa shamba


hilo ni safi muda wote na kuiweka katika hali kutengenezeka kwa
muda wote wa mkataba huu.

6.

Kwamba Mmiliki anayo haki ya kufika katika shamba hilo muda


wowote kwa madhumuini ya kuangalia, kufanya shughuli yoyote au
kukagua hali ya shamba hilo muda wowote bila kutoa taarifa yoyote.

7.

Kwamba Mmiliki ana haki ya kusitisha mkataba huu kwa kumpa


mtunzaji notisi ya wiki moja ambayo ni lazima mtunzaji akubali.

8.

Kwamba endapo kutatokea mgogoro wowote kuhusu mkataba huu,


mgogoro huo utawasilishwa kwa msuluhishi ambaye anakubalika na
pande zote mbili na ambaye uamuzi wake utaheshimiwa na
kutekelezwa bila masharti. Endapo mgogoro hautasuluhishwa, upande
wowote una uhuru wa kuwasilisha mgogoro kwenye vyombo vya sheria.
MKATABA HUU umetiwa
inavyoonekana hapa chini.

saini

na

pande

zote

MMILIKI kwa niaba ya WINNERS Group:


Jina: _____________________
Cheo:_____________________
Tarehe:____________________
Sahihi:____________________
Jina: ______________________
Cheo:______________________
Tarehe: ____________________
Sahihi:_____________________
MTUNZAJI
Jina: ______________________
Cheo:______________________
Tarehe: ____________________
Sahihi:_____________________
Mbele yangu leo hii tarehe, . Mwezi .............. 2013

mbili

kama

_______________________
KAMISHNA WA VIAPO

MKATABA WA KUTUNZA SHAMBA

BAINA YA

WINNERS GROUP

NA

.................................

You might also like