Professional Documents
Culture Documents
Katika sekta ya elimu serikali imetenga kiasi cha Shilingi Milioni 500 kwa ajili ya halmashauri 80
kujenga nyumba za walimu. Kiasi kama hiki kilitengwa katika bajeti ya mwaka 2013/2014 kwa
halmashauri 40 nchini. Tunahoji pesa hizo zilizotumika zilijenga nyumba ngapi na katika halmashauri
zipi na zenye ubora gani? Je upo wapi mkakati wa ujenzi wa mabweni, kuboresha mazingira ya
kufundishia na vifaa vya kujifunzia, na mazingira wezeshi kwa watu wenye ulemavu?
Mwisho tumesikitishwa sana kuona Waziri wa Fedha akikiri bungeni kwamba sera zetu za kiuchumi
zinatokana na mashirika makubwa ya kibeberu kama vile IMF kupitia mpango wa Policy Support
Instrument (PSI). Hali hii inathibitisha kwamba mipango mingi iliyopo nchini haitokani na wananchi bali
matakwa ya mashirika makubwa yanayoendeleza ulimbikizaji kiporaji wa rasilimali nchini. Lakini pia
serikali inaendelea kupuuza utaalamu wa wataalamu wa uchumi wa ndani ya nchi.
Madai
Kutokana na uchambuzi ulioainishwa hapo juu tunadai yafuatayo:
1. Kuwepo mfumo shirikishi na endelevu katika kutengeneza na kufatilia utekelezaji wa bajeti ya
taifa na serikali za mitaa kwa kuzingatia vipaumbele vya wananchi, wanawake na wanaume na
makundi yaliyoko pembezoniMisamaha ya kodi katika kilimo ilenge kuwanufaisha wakulima
wadogo wadogo na sio wawekezaji wakubwa.
2. Kukua kwa uchumi wa nchi kuende sanjari na kupunguza umaskini kwa wananchi wote
wanawake na wanaume na makundi mengine yaliyoko pembezoni.
3. Sekta ya afya ipewe kipaumbele kama zilivyo sekta nyingine katika Mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa (BRN) na kuhakikisha bajeti inafikia 15% ya bajeti ya taifa kama ilivyoagizwa
katika azimio la Abuja.
4. Uwajibikaji zaidi katika ukusanyaji na usimamizi wa mapato na matumizi ya serikali ikiwemo
kuondoa misamaha ya kodi isiyokuwa na tija pamoja na utoaji wa fedha kwa wizara, taasisi na
halmashauri kwa wakati na kiwango stahiki.
Tamko hili limetolewa na:
Sisi wanaharakati wa kikundi kazi cha uchambuzi wa bajeti, wanaharakati kutoka Dar es Salaam, Mbeya,
Morogoro, Shinyanga, Mara na washiriki wa Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS),kwa ushirikiano na
TGNP Mtandao
Imesainiwa na:
Gloria Shechambo,
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji
TGNP Mtandao
Tarehe 12 Juni 2015
4