Professional Documents
Culture Documents
Hatua ya Serikali kutenga fedha hizo itasaidia kupunguza mapungufu ya sare za askari
wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji yaliyokuwa yakilikabili Jeshi hilo na hivyo kuwafanya
askari wake kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Kamishna Jenerali Andengenye amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita
wa 2016/2017 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitenga pia kiasi cha
shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ununuzi wa magari ya kuzima moto, jitihada hizi za Serikali
zinalenga kuondoa changamoto ya uhaba wa vitendea kazi na hivyo kurahisisha
utendaji kazi wa jeshi hilo.