Professional Documents
Culture Documents
OFISI YA RAIS
Simu Na: +255 (026) 2963630 Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Nukushi: +255 (026) 2963629 na Utawala Bora,
Barua Pepe: ps@utumishi.go.tz Jengo la Taaluma Na. 1,
Tovuti: http://www.utumishi.go.tz Chuo cha Masomo ya Biashara na Sheria,
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM),
Barabara ya Mkalama,
S.L.P. 670,
40404 DODOMA.
Waziri Kairuki (Mb) amesema hayo leo katika kikao kazi na Watumishi wa
Umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Tarafa ya Ukonga, kilichofanyika
ukumbi wa mikutano wa shule ya Sekondari ya Pugu, jijini Dar es Salaam.
Aidha, Waziri Kairuki amesema Serikali inaendelea kupitia muundo wake upya
ili kupunguza ukubwa, kuunganisha taasisi zinazofanya kazi zinazofanana na
kuleta uwiano sawa wa stahili kwa watumishi wa umma serikalini.
Ameongeza kuwa Serikali ina nia nzuri na inaijali rasimaliwatu yake ambapo
katika zoezi hili tathmini ya kazi inafanyika ili kila kada itendewe haki katika
kupata stahili kulingana na majukumu yake.
Waziri Kairuki katika ziara yake amewataka watumishi kufanya kazi kwa
ushirikiano na kuwasisitiza Maafisa Utumishi kuwasikiliza wateja wao,
wakiwamo watumishi wenzao na kuwapatia huduma stahiki ikiwa ni pamoja na
kuwaelemisha kuhusu nyaraka za kiutumishi.
2
Awali akisoma taarifa ya Tarafa ya Ukonga, Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Manispaa ya Ilala, Bw. Msongela Palela amempongeza Mhe, Kairuki kwa
kufanya ziara hizo kwani imewasaidia watumishi wa umma kujua masuala
mengi ya kiutumishi.
Mimi nina mwaka mmoja tangu niingie Halmashauri ya Manipaa ya Ilala lakini
kwa ziara hizi nimejifunza masuala mengi sana ya kiutumishi na hata kwa
watumishi wenzangu nina hakika malalamiko mengi yatapungua, Bw. Palela