Professional Documents
Culture Documents
Ni hitajio la kisheria kwa kila raia wa kigeni anayeingia na kutoka nchini kukaguliwa
ili kujiridhisha iwapo hakuna dosari zozote za Uhamiaji, Ulinzi na Usalama.
Sheria ya Uhamiaji inaitaka Idara ya Uhamiaji kumhoji mtu yeyote awe raia wa
Tanzania au kigeni bila kujali anafanya kazi kwenye Kampuni au Shirika gani, pale
inapotaka kujiridhisha juu ya uhalali wa ukaazi wake hapa nchini na ikijiridhisha kuwa
mtu huyu hana dosari zozote inamwachia huru kama ilivyofanyika kwa wafanyakazi
wa Kampuni ya Madini ya Acacia waliohojiwa na kuruhusiwa kuendelea na safari yao
hivi karibuni.
Idara ya Uhamiaji inapenda kuuarifu Umma kuwa hakuna sababu zozote nje ya
matakwa ya Sheria ya Uhamiaji zinazopelekea Idara ya Uhamiaji kuweka kizuizi cha
kuja au kutoka kwa wafanyakazi wa kigeni wa Acacia.
Imetolewa na
Ally M. Mtanda
Msemaji wa Idara ya Uhamiaji
29 Julai 2017