You are on page 1of 1

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI


JESHI LA POLISI TANZANIA

Anuani ya Simu MKUUPOLISI Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi,


Simu : (022) 2110734 Makao Makuu ya Polisi,
Fax Na. (022) 2135556 S.L.P. 9141,
DAR ES SALAAM .

24/08/2017
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini I GP Simon Nyakoro Sirro amemteua Naibu Kamishna wa
Polisi (DCP) Juma Yusuf Ally kuwa Kaimu Kamishna wa Polisi Zan zibar.

Uteuzi huo unafuatia kustaafu kwa aliyekuwa kamishna wa Polisi Zanzibar Kamishna
Hamdani Omari Makame kwa mujibu wa sheria baada ya kuti miza umri wa miaka sitini
(60).

Kabla ya uteuzi huo DCP Juma alikuwa ni Mkuu wa Utawala na Fedha Makao Makuu ya
Polisi Zanzibar.

IGP Sir r o pia amemteua Kamishna Msaidiz i Mwandamizi wa Polisi (SACP ) Lazaro
Mambosasa kuwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam . Kabla ya uteuzi huo,
SACP Mambosasa alikuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.

Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Kaimu Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam
anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara , na aliyekuwa Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Mt wara Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Neema Mwalimu
Mwanga anakwenda Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam .

IGP Sirro pia amemteua aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Gilles Bilabay e Mroto kuwa Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Dodoma na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Emmanuel Lukula
kwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke.

Kabla ya uteuzi huo, ACP Lukula alikuwa Afisa Mnadhimu wa Polisi mkoa wa Mbeya.

Jeshi la Polisi lin atoa wito kwa wananchi wote kuendela kushirikiana na Jeshi hilo kwa
kufichua ta arifa za uhalifu na wahalifu ili kwa pamoja tuendelee kuiweka Tanzania
salama.

Imetolewa na :
Barnabas David Mwakalukwa - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi.
S.L.P 9141
Dar es Salaam
Baruapepe habariphq@yahoo.com

www.policeforce.go.tz www.facebook.com/tanpol www.twiter.com/tanpol

You might also like