Professional Documents
Culture Documents
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inatoa pongezi za dhati kwa
watoto wote waliopata ufaulu wa juu na kushika nafasi 10 bora kitaifa katika matokeo ya mtihani
wa Darasa la Saba kwa mwaka 2017.
Aidha, kwa namna ya pekee Wizara inawapongeza wanafunzi 4 wa kike waliopata ufaulu wa juu
na kuingia kwenye ushindani wa nafasi kumi bora kwa mwaka huu wa 2017, ukilinganisha na
mwanafunzi 1 tu wa kike aliyengara katika nafasi hizo kwa mwaka 2016.
Wizara imetambua juhudi binafsi zilizofanywa na mwanafunzi wa kike Hadija A. Ally kutoka
Shule ya Msingi Sir John ya jijini Tanga, ambaye ameshika nafasi ya kwanza kati ya wanafunzi
10 hodari kitaifa. Aidha, Wizara inampongeza mwanafunzi aliyeshika nafasi ya pili, Naseem K.
Said (Sir John, Tanga), nafasi ya sita ikishikiliwa na Insiya Kalimuddin (Sir John Tanga), na
nafasi ya saba ikishikilikiwa na Colletha Masungwa wa St. Achileus, ya mkoani Kagera.
Taarifa ya TECTA inaonesha kuwa ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 70.3 ya mwaka 2016
hadi asilimia 72.76 kwa mwaka 2017, sawa na ongezeko la asilimia 2.4; huu ni ushuhuda thabiti
kuwa wadau wa watoto wameshirikiana na Serikali katika kuimarisha na kuboresha mazingira ya
watoto kupata haki ya kuendelezwa na kumwezesha Mtoto wa kike na wa kiume kutimiza ndoto
zake.
1
Wizara inawataka watoto wote wa kike na wa kiume waelewe kuwa wamehitimu daraja moja, na
bado wanalojukumu la kujiendeleza zaidi katika masomo ya sekondari na kwa wale ambao
hawakupata ufaulu unaotosheleza wanayo nafasi ya kujiendeleza kupitia taaluma mbalimbali na
stadi za maisha ili kupata maarifa yatakayowawezesha kutoa mchango katika juhudi za kufikia
uchumi wa kati na wa viwanda.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, WAZEE NA WATOTO
25/10/2017