Professional Documents
Culture Documents
Ameongeza kuwa ni wajibu wa wakala huo kupitia nyumba hizo kila wakati ili kufahamu
nyumba chakavu na kuweka mikakati ya kuzikarabati ili kuokoa fedha nyingi ambazo
zinatumika katika ukarabati wa mara moja kwa nyumba nyingi.
Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TBA, Steven Simba, amemuhakikishia Naibu Waziri
Kwandikwa kuwa TBA imejipanga kuhakikisha kuwa nyumba za Serikali zinajengwa kwa
kuzingatia viwango kulingana na mahitaji.
Awali akitoa taarifa kwa Naibu Waziri Kwandikwa amemueleza kuwa mwanzoni
walikua na nyumba mia nne, lakini sasa wameongezewa nyumba nyingine mia nne
kutoka CDA na pia kuna miradi inaendelea ya ujenzi wa nyumba nyingine, hivyo uwepo
wa nyumba hizo utapunguza changamoto ya makazi kwa watumishi wanaohamia
mkoani humo.