Simu: 255-22-2114512, 2116898 OFISI YA RAIS, E-mail: press@ikulu.go.tz IKULU, 1 BARABARA YA BARACK OBAMA, Tovuti : www.ikulu.go.tz 11400 DAR ES SALAAM. Faksi: 255-22-2113425 Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ikulu, Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Siza Donald Tumbo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Utawala ya Chuo cha Ufundi Arusha (Arusha Technical College – ATC).
Prof. Tumbo ni Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Zana za Kilimo na
Teknolojia Vijijini (Center for Agricultural Mechanization and Rural Technology – CAMARTEC). Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Mhandisi Mussa Iyombe kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (Public Service Social Security Fund - PSSSF).
Uteuzi huu wa wenyeviti wa bodi umeanza tarehe 13 Mei, 2018.
Gerson Msigwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU Dar es Salaam 14 Mei, 2018