Professional Documents
Culture Documents
1
Kwa mfano inakadiriwa kwamba Tanzania inapoteza takribani dola za
kimarekani milioni 531.5 kila mwaka kutokanana misamaha ya kodi.
Aidha warsha hii ilibaini kuwa baadhi ya mikataba mbalimbali ya kodi ina
vifungu ambavyo vinainyima uwezo serikali yetu kukusanya kodi kwa
makampuni ya nje chini sheria ya kodi ya mwaka 2004.
Pia warsha hii ilibaini kuwa wananchi hawana uelewa wa kutosha kuhusu
kodi zinazotozwa kwa makampuni ya nje yanayofanya kazi Tanzania, na hii
inachangiwa zaidi na changamoto za usiri katika maswala ya fedha. Pia
imeshauriwa kwamba mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) iwengezewe
uwezo ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi katika kukusanya
kodi .