You are on page 1of 1

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

BUNGE LA TANZANIA
Tele: +255 026 2322761-5 Ofisiya Bunge
Fax No. +255 026 2324218 S.L.P. 941
E-mail: cna@bunge.go.tz DODOMA.

TAARIFA KWA UMMA

Kamati ya Bunge ya Bajeti kwa mujibu wa Kanuni ya 117 (9), imepanga kufanya
mkutano wa kusikiliza maoni ya wadau wote wa masuala ya fedha (Public
Hearing) kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2019 (The Finance
Bill, 2019).

Mkutano huo wa kusikiliza na kupokea maoni ya wadau (Public Hearing)


unatarajiwa kufanyika siku ya Alhamisi tarehe 20 na Ijumaa tarehe 21, 2019
kuanzia saa Nne Asubuhi katika Ukumbi wa Pius Msekwa Jijini Dodoma.

Kwa kuzingatia umuhimu wa Muswada huo, Kamati inawaalika wadau wote


kufika na kuwasilisha maoni yao kabla Muswada huo haujapelekwa katika
hatua nyingine. Maoni ya wadau yanaweza pia kuwasilishwa kwa njia ya Posta
au Baruapepe kwa anuani ifuatayo:-

Katibu wa Bunge,
Ofisi ya Bunge,
S.L.P. 941,
DODOMA.

Baruapepe: cna@bunge.go.tz

Muswada huo pia unaweza kupakuliwa kupitia tovuti ya Bunge,


www.parliament.go.tz

Imetolewa na: Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa,


Ofisi ya Bunge,
S.L.P 941,
DODOMA.

17 Juni, 2019.

You might also like